Katika ulimwengu tulioao tunapita katika vipindi tofauti, na vipindi hivyo vina makusudi kwa Mungu.Kuna wakati wa kufurahi na wakati wa kulia, kuna wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna. Watu wengi tunatazamia na tunapenda kufurahi kila wakati tule tunywe na kupata kila jema kutoka kwa Mungu lakini tunajikuta tunakumbana na nyakati tofauti hii ni kwasababu MUNGU ameweka kila wakati kwa makusudi yake.
Makusudi ya vipindi tofauti tunavyopitia wakati mwingine imekuwa fumbo kwa muhusika isipokuwa Mungu hutambua hilo maana ameamuru, na sihivyo tu wakati mwingine tunatambua kusudi la Mungu baada ya kuona matokeo.
Jambo la msingi hapo ni kwamba tunatakiwa kujua kuwa katika kila wakati ambao Mungu anatupitisha tukazane kulijua na kulifuatilia kusudi la MUNGU ni nini haswa.Itatusaidia kujiepusha kwa mabaya yatakayotutoa uweponi mwa MUNGU....MUHUBIRI 3;1-7
No comments:
Post a Comment