Tuesday, 10 March 2015

KUOMBA KWA IMAN

Kiufupi Iman ni ni kuwa na uhakika wa  matarajio  ulionayo, akili na ufahamu wako  vinapata    picha halisi ya yale uyatarajiayo

 Kwa kawaida tunajua kuwa mwanadamu lazima uishi ukiwa na matarajio fulan fulani kulingana na wakati na hali halisi ya mambo. Kwa habari ya imani UHAKIKA  ni lazima .

Mgonjwa anapokunywa dawa ni matarajio yake kupona na kwakuwa huwa na matarajio mema yanambidisha  anywe kwa bidii ili apone.Alokata tamaa  hata dozi hawezi kumaliza maana hana uhakika wa kupona.

  Basi iman ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana  ya  mambo yasiyoonekana Ebr 11;1..


Unapoenda mbele za Mungu omba huku ukitarajia kupata kile unachokihitaji { Amwendeaye Mungu lazima aamini Ebr  11;6 } Kwa kutokuamin, kutakufanya usiombe kwa bidii maana huna matarajio mema .

Kuomba kwa imani kutakufanya umtafute sana Mungu na  sio miujiza maana wenigne kwa kutafuta miujiza wameingia ktk mambo yanayowajutisha na kuwaondolea amani. Muujiza au jambo unalolitaka Mungu aweza tenda kwa namna isiyo fikirika maana yeye hakaririki, muujiza mmoja huutenda kwa namna mbalimali si lazima alivyopokea mwenzio ndivyo utapokea, Omba kwa imani.

Kwa imani utaaumba mambo mema kwaajili yako

Kwa imani utaponywa/  utaepushiwa uharibifu na kufanywa mrithi wa haki. 

Kwa imani utatimiziwa haja ya moyo wako . 

utapita na kuishi mahali  paliposhindikana .

Kwa imani utatambua  vikwazo vya mafanikio yako.                

Kwa imani utamshinda adui

Kwa imani utapata familia bora  nk

Sunday, 8 March 2015

KUMCHA MUNGU







Kumcha Mungu, twaweza kueleza  kwa namna mbalimbali kulingana na mtu anavyoelewa .Kumcha
MUNGU ni zaidi ya  kuonesha  unyenyekevu wa hali ya juu sana mbele za  MUNGU.

  EBR  12; 28-29  Basi kwakuwa tunapokea ufalme  usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza , pamoja na unyenyekevu na kicho. Maaana Mungu wetu ni moto ulao.

 Jambo hili  la  kumcha  Mungu   linaweza kudhihirika ktk ibada au hata maisha ya kila siku . Hata hivyo kwaajili hii   twaweza kutofautisha wacha Mungu na  wasio  wacha . Mcha Mungu ametambua uwepo wa Mungu na  nguvu zake   , hukumu ya Mungu na mambo mengine ambayo humfunua MUNGU  kwake . kila mtu liko jambao  au mambo yanayomfanya atambue  uwepo wa Mungu na hukumu yake na hilo laweza kuwa sababu ya kumcha Mungu.
Zaid sana tutambue kuna ufalme usiotetemeshwa na kuyumbishwa ,hudumu hata milele . Kama falme za dunia tunaziheshimu bas uflme huu ni zaidi maana Mungu mwenyewe ni mtawala.


UBARIKIWE.

Sunday, 18 January 2015

KUKUMBUKWA NA MFALME


Wafalme ama marais wa dunia hii wana mambo mengi na makubwa na aghalabu si rahisi kuwakumbuka watu wa chini.
Kwa wakristo mfalme wetu ni Mungu mkuu na Yesu Kristo ambay kamwe hasahau wanaomkimbilia.
2Samweli 9:1—13
1 Kisha Daudi akasema, Je! Amesalia mtu mmoja katika nyumba ya Sauli, nipate kumtendea mema kwa ajili ya yonathani?
Kwa muhtasari hii habari ya Mefibosheti kukumbukwa na Mfalme Daudi, Mefibosheti ni wa familia ya adui yake mkubwa Daudi, mfalme Sauli. Kwenye mstari wa 8 unasema ‘akasujudu, akasema mimi mtumwa wako ni nini, hata ukamwangalia MBWA MFU kama mimi?
Mefibosheti amekata tamaa kiasi cha kujifananisha na MBWA MFU. Mpendwa mbwa afapo huwa hakumbukwi na yeyote, mzoga wa Mbwa hupitiwa mbali na zaidi labda lipite gari la taka liuchukue dampo... na hivyo ndivyo anajiona Mefibosheti mbele ya mfalme.
Mefibosheti amekata tamaa kwa sababu;
1. Ni mlemavu na kwa desturi ya wayahudi anaonekana ni laana na hivyo kutengwa.
2. Ni mjukuu wa Sauli mfalme aliyeasi na kizazi chake chote kupukutika.
3. Mfalme Daudi alikuwa adui wa Sauli
4. Mefibosheti ni maskini sana si tu ulemavu bali ufukara.
Mefibosheti anapokumbukwa na mfalme kila kitu kinabadilika;
1. Kaitwa mezani pa mfalme. Hebu tufananishe mezani pa mfalme na mezani pa rais ikulu.
2. Kapewa nafasi ya kula na kunywa mezani pa mfalme (raisi)
3. Akapewa milki yote ya Sauli... kumbuka sauli alikuwa mfalme na mwenye utajiri mkubwa.
4. Kapewa wafanyakazi 36 yaani 1+15+20 kwa Siba, wanawe 15 na watumwa 20 wa siba
5. Akapewa haki ya kufanyika mwanamfalme (prince) wa Daudi.
Kristo anapokukumbuka anakukaribisha ule mezani pake, anakupa milki (mali), wafanyakazi na haki ya kufanyika mwanamfalme(Prince).

Mpendwa yapaswa sana kung’ang’ania sana kwa Mungu ili tukumbukwa kwani Mugnu hatazami tukoje na tunamiliki nini bali anaangalia tunavyoweza kushukwa kwake namna tunavyojiona si kitu bali yeye ndiye mwenye thamani na kila kitu kwetu

Nakutakia maisha ya imani na ushindi...

Bidii siri ya mafanikio

Mhu 9;10a
"Lolote mkono wako utakalopata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako;"

Watu wengi hawapendI umasikin na wakati mwingine kuwa na maombi ya kuutokomeza lakini pasipo kufanya kazi ni sawa na mtu asiye na maono.
Bidii siri ya mafanikio

Thursday, 15 January 2015

Karibu

Bwana Yesu asifiwe

Mpendwa ninayo furaha kukukaribisha kwenye blogu yetu mpya ya Betheli Halisi. Lengo la blogu hii ni kuchapisha neno na masomo ya kiroho kwa ujumla, maneno yatakayomfanya mkristo aishi maisha ya imani na ushindi.

Chanzo cha jina la blogu hii ni kutoka Mwanzo 28:17-19
17  Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni.
18  Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.
19  Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu. 


Karibu sana
 
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwafunike

wenu 
Mwl. Mary