Katika ulimwengu tulioao tunapita katika vipindi tofauti, na vipindi hivyo vina makusudi kwa Mungu.Kuna wakati wa kufurahi na wakati wa kulia, kuna wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna. Watu wengi tunatazamia na tunapenda kufurahi kila wakati tule tunywe na kupata kila jema kutoka kwa Mungu lakini tunajikuta tunakumbana na nyakati tofauti hii ni kwasababu MUNGU ameweka kila wakati kwa makusudi yake.
Makusudi ya vipindi tofauti tunavyopitia wakati mwingine imekuwa fumbo kwa muhusika isipokuwa Mungu hutambua hilo maana ameamuru, na sihivyo tu wakati mwingine tunatambua kusudi la Mungu baada ya kuona matokeo.
Jambo la msingi hapo ni kwamba tunatakiwa kujua kuwa katika kila wakati ambao Mungu anatupitisha tukazane kulijua na kulifuatilia kusudi la MUNGU ni nini haswa.Itatusaidia kujiepusha kwa mabaya yatakayotutoa uweponi mwa MUNGU....MUHUBIRI 3;1-7
Monday, 27 June 2016
MPANGO WA MUNGU
Mungu kama aisivyo ni Mungu wa mipango,tangu mwanzo Mungu amekuwa akienda kwa mipango. ukisoma kitabu cha mwanzo 1; Mungu alikuwa na mpango wa kuijaza dunia maana ilikuwa utupu na kuiptia Adamu na Hawa dunia ikipata vizazi tofautitofauti.
Napenda tujikumbushe mpango wa Mungu ktk agano jipya Mungu anakusudia kuleta wokovu kwa mwanadamu baaada ya uasi, jambo ambalo Mungu alilifanya kurudisha mahusiano yake na mwanadamu ni kumtoa mwanae wa pekee Yohana 3;16-19. Wokovu ni mpango kamili wa Mungu kumkomboa mwanadamu, hakuna mwanadamu anaeweza kupata msamaha wa dhambi isipokuwa kwa njia ya kuukubali wokovu.
Jinsi ya kuupata wokovu, ni kwanjia ya kumkiri yesu kwa kinywa chako Warumi 9;10 , na ukiri wako unadhihirisha kile ulichokiamini moyoni mwako. Kumwamini yesu yakuwa ni Bwana na mwokozi katika maisha yako maana kwa yeye wokovu unapatikana.
Ikiwa wokovu ndo mpango sahihi wa kumuokoa mwanadamu, hatutapona jehanamu bila huo japokuwa jambo la jehanamu limeonekana kuwa jambo la kufikirika lakini hukumu ipo kama vile tunavoamini kifo kipo tujitayarishe kukabiliana nayo...
NAWAPENDAAA
Napenda tujikumbushe mpango wa Mungu ktk agano jipya Mungu anakusudia kuleta wokovu kwa mwanadamu baaada ya uasi, jambo ambalo Mungu alilifanya kurudisha mahusiano yake na mwanadamu ni kumtoa mwanae wa pekee Yohana 3;16-19. Wokovu ni mpango kamili wa Mungu kumkomboa mwanadamu, hakuna mwanadamu anaeweza kupata msamaha wa dhambi isipokuwa kwa njia ya kuukubali wokovu.
Jinsi ya kuupata wokovu, ni kwanjia ya kumkiri yesu kwa kinywa chako Warumi 9;10 , na ukiri wako unadhihirisha kile ulichokiamini moyoni mwako. Kumwamini yesu yakuwa ni Bwana na mwokozi katika maisha yako maana kwa yeye wokovu unapatikana.
Ikiwa wokovu ndo mpango sahihi wa kumuokoa mwanadamu, hatutapona jehanamu bila huo japokuwa jambo la jehanamu limeonekana kuwa jambo la kufikirika lakini hukumu ipo kama vile tunavoamini kifo kipo tujitayarishe kukabiliana nayo...
NAWAPENDAAA
Tuesday, 10 March 2015
KUOMBA KWA IMAN
Kiufupi Iman ni ni kuwa na uhakika wa matarajio ulionayo, akili na ufahamu wako vinapata picha halisi ya yale uyatarajiayo
Kwa kawaida tunajua kuwa mwanadamu lazima uishi ukiwa na matarajio fulan fulani kulingana na wakati na hali halisi ya mambo. Kwa habari ya imani UHAKIKA ni lazima .
Mgonjwa anapokunywa dawa ni matarajio yake kupona na kwakuwa huwa na matarajio mema yanambidisha anywe kwa bidii ili apone.Alokata tamaa hata dozi hawezi kumaliza maana hana uhakika wa kupona.
Basi iman ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana Ebr 11;1..
Unapoenda mbele za Mungu omba huku ukitarajia kupata kile unachokihitaji { Amwendeaye Mungu lazima aamini Ebr 11;6 } Kwa kutokuamin, kutakufanya usiombe kwa bidii maana huna matarajio mema .
Kuomba kwa imani kutakufanya umtafute sana Mungu na sio miujiza maana wenigne kwa kutafuta miujiza wameingia ktk mambo yanayowajutisha na kuwaondolea amani. Muujiza au jambo unalolitaka Mungu aweza tenda kwa namna isiyo fikirika maana yeye hakaririki, muujiza mmoja huutenda kwa namna mbalimali si lazima alivyopokea mwenzio ndivyo utapokea, Omba kwa imani.
Kwa imani utaaumba mambo mema kwaajili yako
Kwa imani utaponywa/ utaepushiwa uharibifu na kufanywa mrithi wa haki.
Kwa imani utatimiziwa haja ya moyo wako .
utapita na kuishi mahali paliposhindikana .
Kwa imani utatambua vikwazo vya mafanikio yako.
Kwa imani utamshinda adui
Kwa imani utapata familia bora nk
Sunday, 8 March 2015
KUMCHA MUNGU
Kumcha Mungu, twaweza
kueleza kwa namna mbalimbali kulingana na mtu anavyoelewa .Kumcha
MUNGU ni zaidi ya
kuonesha unyenyekevu wa hali ya juu sana mbele za MUNGU.
EBR 12;
28-29 Basi kwakuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe
na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza , pamoja na
unyenyekevu na kicho. Maaana Mungu wetu ni moto ulao.
Jambo hili
la kumcha Mungu linaweza kudhihirika ktk ibada au hata
maisha ya kila siku . Hata hivyo kwaajili hii twaweza kutofautisha
wacha Mungu na wasio wacha . Mcha Mungu ametambua uwepo wa Mungu
na nguvu zake , hukumu ya Mungu na mambo mengine ambayo
humfunua MUNGU kwake . kila mtu liko jambao au mambo yanayomfanya
atambue uwepo wa Mungu na hukumu yake na hilo laweza kuwa sababu ya
kumcha Mungu.
Zaid sana tutambue kuna ufalme usiotetemeshwa na kuyumbishwa ,hudumu hata milele . Kama falme za dunia tunaziheshimu bas uflme huu ni zaidi maana Mungu mwenyewe ni mtawala.
UBARIKIWE.
Sunday, 18 January 2015
KUKUMBUKWA NA MFALME
Wafalme ama marais wa dunia hii wana mambo mengi na makubwa na aghalabu si rahisi kuwakumbuka watu wa chini.
Kwa wakristo mfalme wetu ni Mungu mkuu na Yesu Kristo ambay kamwe hasahau wanaomkimbilia.
2Samweli 9:1—13
1 Kisha Daudi akasema, Je! Amesalia mtu mmoja katika nyumba ya Sauli, nipate kumtendea mema kwa ajili ya yonathani?
Kwa muhtasari hii habari ya Mefibosheti kukumbukwa na Mfalme Daudi, Mefibosheti ni wa familia ya adui yake mkubwa Daudi, mfalme Sauli. Kwenye mstari wa 8 unasema ‘akasujudu, akasema mimi mtumwa wako ni nini, hata ukamwangalia MBWA MFU kama mimi?
Mefibosheti amekata tamaa kiasi cha kujifananisha na MBWA MFU. Mpendwa mbwa afapo huwa hakumbukwi na yeyote, mzoga wa Mbwa hupitiwa mbali na zaidi labda lipite gari la taka liuchukue dampo... na hivyo ndivyo anajiona Mefibosheti mbele ya mfalme.
Mefibosheti amekata tamaa kwa sababu;
1. Ni mlemavu na kwa desturi ya wayahudi anaonekana ni laana na hivyo kutengwa.
2. Ni mjukuu wa Sauli mfalme aliyeasi na kizazi chake chote kupukutika.
3. Mfalme Daudi alikuwa adui wa Sauli
4. Mefibosheti ni maskini sana si tu ulemavu bali ufukara.
Mefibosheti anapokumbukwa na mfalme kila kitu kinabadilika;
1. Kaitwa mezani pa mfalme. Hebu tufananishe mezani pa mfalme na mezani pa rais ikulu.
2. Kapewa nafasi ya kula na kunywa mezani pa mfalme (raisi)
3. Akapewa milki yote ya Sauli... kumbuka sauli alikuwa mfalme na mwenye utajiri mkubwa.
4. Kapewa wafanyakazi 36 yaani 1+15+20 kwa Siba, wanawe 15 na watumwa 20 wa siba
5. Akapewa haki ya kufanyika mwanamfalme (prince) wa Daudi.
Kristo anapokukumbuka anakukaribisha ule mezani pake, anakupa milki (mali), wafanyakazi na haki ya kufanyika mwanamfalme(Prince).
Mpendwa yapaswa sana kung’ang’ania sana kwa Mungu ili tukumbukwa kwani Mugnu hatazami tukoje na tunamiliki nini bali anaangalia tunavyoweza kushukwa kwake namna tunavyojiona si kitu bali yeye ndiye mwenye thamani na kila kitu kwetu
Nakutakia maisha ya imani na ushindi...
Bidii siri ya mafanikio
Mhu 9;10a
"Lolote mkono wako utakalopata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako;"
Watu wengi hawapendI umasikin na wakati mwingine kuwa na maombi ya kuutokomeza lakini pasipo kufanya kazi ni sawa na mtu asiye na maono.Bidii siri ya mafanikio
"Lolote mkono wako utakalopata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako;"
Watu wengi hawapendI umasikin na wakati mwingine kuwa na maombi ya kuutokomeza lakini pasipo kufanya kazi ni sawa na mtu asiye na maono.Bidii siri ya mafanikio
Thursday, 15 January 2015
Karibu
Bwana Yesu asifiwe
Mpendwa ninayo furaha kukukaribisha kwenye blogu yetu mpya ya Betheli Halisi. Lengo la blogu hii ni kuchapisha neno na masomo ya kiroho kwa ujumla, maneno yatakayomfanya mkristo aishi maisha ya imani na ushindi.
Chanzo cha jina la blogu hii ni kutoka Mwanzo 28:17-19
17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni.
18 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema,
akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha
kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake.
19 Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
Karibu sana
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwafunike
wenu
Mwl. Mary
Subscribe to:
Comments (Atom)