Sunday, 8 March 2015

KUMCHA MUNGU







Kumcha Mungu, twaweza kueleza  kwa namna mbalimbali kulingana na mtu anavyoelewa .Kumcha
MUNGU ni zaidi ya  kuonesha  unyenyekevu wa hali ya juu sana mbele za  MUNGU.

  EBR  12; 28-29  Basi kwakuwa tunapokea ufalme  usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza , pamoja na unyenyekevu na kicho. Maaana Mungu wetu ni moto ulao.

 Jambo hili  la  kumcha  Mungu   linaweza kudhihirika ktk ibada au hata maisha ya kila siku . Hata hivyo kwaajili hii   twaweza kutofautisha wacha Mungu na  wasio  wacha . Mcha Mungu ametambua uwepo wa Mungu na  nguvu zake   , hukumu ya Mungu na mambo mengine ambayo humfunua MUNGU  kwake . kila mtu liko jambao  au mambo yanayomfanya atambue  uwepo wa Mungu na hukumu yake na hilo laweza kuwa sababu ya kumcha Mungu.
Zaid sana tutambue kuna ufalme usiotetemeshwa na kuyumbishwa ,hudumu hata milele . Kama falme za dunia tunaziheshimu bas uflme huu ni zaidi maana Mungu mwenyewe ni mtawala.


UBARIKIWE.

No comments:

Post a Comment